
FAIDA ZA JUISI YA UKWAJU.
- Chanzo kizuri cha viuasumu mwilini 'antioxidants' ambavyo huzuia Saratani (cancer)
- Chanzo cha Vitamini B na C vile vile "carotentes"
- Hushusha joto la mwili na kuondosha homa, hasa homa ya malaria na homa ya matumbo
- Huulinda mwili dhidi ya mafua na kero za mafua kooni
- Husaidia myeyusho na mmengenyo wa chakula na kuondosha kuvimbiwa
- Husaidia kutibu matatizo ya nyongo (bile disorders)
- Husaidia kurahisisha choo (laxative)
- Husaidia kupunguza wingi wa lehemu (cholesterol) na hivyo kuimarisha moyo
- Husaidia ngozi kuwa nyororo, vile vile husaidia ngozi inayopona baada ya kuungua au yenye vidonda
- Husaidia kuua minyoo tumboni (kwa watoto wadogo)
MAPARACHICHI PEA (AVOCADO)
Ndani ya tunda hili kuna maji kiasi kidogo sana
ukilinganisha na matunda mengine lakini kuna mafuta mengi na unaweza
kuchanganya kula na tunda lingine kama vile apple, ndizi, chungwa au
hata maziwa kwa kutengeneza juisi.
TINDIKALI
Licha ya kuwa na mafuta parachichi lina tindikali (acid) mbalimbali
ikiwemo inayojulikana kama amino ambayo husaidia sana kukinga na kutibu
maradhi katika mwili wa binadamu. Tunda hili pia lina protini ya
kiwango cha juu.
Pia kuna tindikali inayoitwa oleic acid kwenye parachichi ambayo husaidia kukinga magonjwa ya moyo, kiharusi na kansa.
VITAMINI “E” NA B6
Imeelezwa na wataalamu kuwa tunda hili lina kiwango kikubwa cha vitamini
E kuliko ile inayopatikana kutoka kwenye mazao ya wanyama.Parachichi
lina vitamini hiyo nyingi kuliko inayopatikana katika mayai ambayo
yanasifika kwa kuwa na vitamini e, hivyo hii inathibitisha kuwa lina
faida kubwa mwilini.
Licha ya vitamini E pia ndani ya parachichi kuna vitamini B6 na kuna
madini ya chuma (Iron) kwa wingi na madini ya potassium, pamoja na
vitamin B6 na E mlaji anaweza kuletawa nafuu sana kama alikuwa na
matatizo ya stress, matatizo ya uzazi kama ugumba na jogoo kutopanda
mtungi Nguvu za kiume pia tunda hili linasaidia (impotence) .
FAIDA ZA PARACHICHI
Licha ya binadamu kufaidika na virutubisho vya tunda hili kuna faida
nyingi za parachichi kama vile majani ya mti wake pamoja na magamba,
baadhi ya watu hutumia kutibu maradhi ya kuharisha.
Majani na magamba hayo hutibu pia tatizo la gesi tumboni, kutuliza
kikohozi pamoja na matatizo ya ini na kusafisha njia ya mkojo.
Hata hivyo, kwa mujibu wa wataalamu wa dawa za mitishamba, dawa hii
haifai kutumiwa na wanawake ambao wana mimba kwani wakitumia inaweza
kusababisha kuharibika kwa ujauzito.
HEDHI
Hata hivyo, wataalamu wa tiba mbadala wanasema dawa hiyo inaweza
kuwasaidia sana wanawake ambao wameshindwa kuona siku zao kwa wakati, na
wakitumia vyema wanaweza kuanza kuona siku zao.
Aidha, tunda hili linasaidia uyeyushaji wa chakula tumboni hasa kwa wale
wenye matatizo ya vidonda vya tumbo, kwani parachichi lina nyuzinyuzi
“fiber” ambayo ni muhimu kukinga kuta za utumbo. Watu wenye maradhi ya
anaemia, diabetes, matatizo ya mfumo wa neva, matatizo ya mishipa ya
moyo hasa wa artery wanashauriwa kula tunda hili mara nyingi.
Lakini pia tunda hili limethibitishwa na wataalamu kuwa linapunguza kwa
kiwango kikubwa cholesterol kutoka kwenye damu hasa kwa watu wanene.
Tunda hili husaidia kulainisha ngozi na kuondoa mikunjo, hung`arisha na
kulainisha nywele na kuzisaidia kukua pia kuziimarisha na kuzuia
kukatikakatika.
Parachichi unaweza kulila kwa kulimenya au kwa kulisaga na kutengeneza
juisi na kama nilivyoeleza hapo juu unaweza kuchanganya na matunda
mengine kama tulivyoyataja na hutaharibu virutubisho vilivyomo badala
yake utaongeza ubora wa juisi yako.
Watoto wadogo pia unaweza kuwapa tunda hili na wakafaidika na haya tuliyoyaandika.
Parachichi pia huweza kutumika kama siagi kwa kupaka kwenye mkate au kuchanganya na wali.
Haya wale wanaopenda ngozi zao za mwilini zisijikunje hata wakiwa watu
wazima wadumu kula tunda hili kila siku katika maisha yao basi ngozi za
mwili wao hazitajikunja hata usoni watakuwa kila siku vijana hata
wakiwa wazee.
PAPAI
Watu wengi hulitumia tunda la papai kwa sababu ya utamu wake.
Hata hivyo mbali na kuwa na ladha nzuri, tunda la papai lina faida lukuki kwa afya ya mwanadamu.
UTAJIRI WA VITAMINITunda la papai lina vitamini A,B,C,D, na E jambo linalo liweka tunda hili katika kundi la matunda na vyakula vyenye utajiri mkubwa wa vitamin.
Mti wa papai
FAIDA ZA KIAFYA ZA TUNDA LA PAPAI
Tunda la papai lina faida nyingi sana kwa afya ya mwanadamu. Miongoni mwa faida hizo ni pamoja na kuwa na uwezo wa :
Mbegu za Papai
1. Kutibu tatizo la Shida ya kusaga chakula tumboni
2. Kutibu Udhaifu wa tumbo
3. Kutibu Kisukari na asthma au pumu.
4. Kutibu Kikohozi kitokacho mapafuni
Mizizi Ya Papai
5. Kutibu Kifua kikuu
6. Tunda hili huleta afya nzuri ukitumia kila siku
7. Maziwa yanayotoka katika jani lake huponya vidonda
8. Vilevile yanasaidia kutibu sehemu palipoungua moto
9. Kama hiyo haitoshi, maziwa yanayotoka katika jani la mpapai yanatibu kiungulia na Ugonjwa wa colon (njia ya haja kubwa ndani)
Majani Ya Mpapai
10. Pia yanasaidia kutofunga choo
11. Maganda ya tunda la papai yanasaidia kutibu tatizo la kuungua, vipele na saratani ya ngozi.
12. Mbegu zake zinatibu ini zikitafunwa 10 – 12 kwa siku 5.
13. Majani yake yakaushie ndani, yanatibu pumu. Inapoanza kubana yachome majani yaliyokaushwa kisha jifukize, kule kubanwa kutakisha.
14. Majani yake yanasaidia katika kutibu shinikizo la damu.
15. Papai likimenywa na kupondwa linafaa Sana katika masuala ya urembo kwani linaweza kutumika Kama vile unavyotumia lotion kulainisha uso.
16. Mbegu za papai zina uwezo wa kutibu homa. Meza mbegu za papai kiasi cha kijiko cha chakula mara 3 kwa ajili ya kutibu homa.
17. Mbegu za papai zilizokaushwa ndani kisha zikasagwa kuwa unga zinatibu malaria, tumia kijiko 1 cha chai changanya na uji, kunywa mara 3 kwa siku 5 Mgonjwa wa kifua kikuu akila matunda haya kwa muda mrefu atapona bila dawa nyingine.
18. Mizizi yake ikipondwa na kulowekwa katika maji yaliyochemshwa, lita 2 na nusu kwa dakika 15, yanatibu figo, bladder, yanazuia kutapika. Nusu kikombe cha chai kutwa mara 3 kwa siku 5.
FAIDA ZA NANASI
UTAJIRI WA VITAMINI NA MADINI :
Nanasi ina vitamini
A,B na C na pia ina madini ya chuma, calcium, copper na phosphorous ambayo yote
ni muhimu sana
katika afya ya
mwanadamu.
ii.
Tunda hili husaidia kutengeneza damu
iii.
Nanasi husaidia
kuimarisha mifupa , meno, neva na misuli (muscles).
iv.
Tunda
la nanasi hutibu matatizo ya tumbo.
v.
Hutibu matatizo
ya Bandama
vi.
Hutibu matatizo
ya Ini
vii.
Husaidia kusafisha
Utumbo mwembamba
viii.
Husaidia kutibu Homa
ix.
Husaidia kutibu Vidonda mdomoni
x.
Husaidia kutibu
Magonjwa ya koo
xi.
Husaidia kutibu
tatizo la Kupoteza kumbukumbu
xii.
Husaidia kutibu
maradhi ya akili Kukosa mori (low spirit)
xiii.
Husaidia kutibu
Kikohozi
xiv.
Husaidia kutibu
tatizo la Kutetemeka
xv.
Husaidia kutibu
tatizo la Woga ( Anxiety )
xvi.
Husaidia kutibu matatizo ya wanawake (upungufu wa hormones au
makosa fulani katika sehemu za siri )
xvii. Huondoa shida ya kufunga choo
xviii.
Hutibu tatizo
la baridi yabisi
xix.
Husaidia katika
kutibu tatizo la
Upungufu wa damu
xx.
Pia
tunda hili huwasaidia
akina mama wanaonyonyesha (wenye maziwa machache)
No comments:
Post a Comment